UTANGULIZI. Shalom marafiki wa Yesu, Kwanza kabisa nimshukuru Mungu kwa nafasi hii ya kipekee ya kupata wasaa wa kutumika katika madhabahu hii, niwashukuru viongozi wa huduma hii kwa mara nyingine tena kutuletea mfululizo wa semina hizi. Kwa wale wageni karibuni na kabla sijaanza basi nitaomba tena uongozi utume ile miongozo kwa faida yetu na wale wageni tujikumbushe.Tafadhali andaa mahala pa kuandika. Na jiandae kwa darasa. Naitwa Victor Jerome, kitaaluma ni mhandisi wa mifumo ya habari na teknolojia ya mtandanio yani information systems and network engineering.Nje ya hapo ni certified life coach, na mentor, muasisi wa huduma ya *teen for teen mentorship program* Huduma inayojihusisha na kuwasaidia vijana kujitambua na kuishi maisha wanayoyatamani na kutimiza ndoto zao za maisha, nimejikita hasa katika masomo ya kujitambua, mindset, purpose,na goal setting. Pia ni mshereheshaji na mwandazi wa shughuli na ninajulikana pia kama mc mtumishi, Kwa sasa naishi mkoani moshi...